Pilau La Noeli

January 22, 2010
By

Pilau la Noeli

Wakati wa Noeli umeisha, lakini kwa sababu wachache wamependelea nitafsiri mapishi yawe kwa Kiswahili. Nimeona ni vizuri nianze na pishi hili maan ni tamu sana. Na pia unaweza kuliandaa wakati wowote wa sherehe yoyote ile. Sasa, kurahisisha mambo, weka makini haya katika viungo

  • kkm – Kikombe / vikombe
  • kjm – Kijiko cha meza / vijiko
  • kjc – Kijiko cha chai / vijiko

Hili ni pilau tamu sana kwa sababu ya mchanganyiko wa korosho, zabibu kavu na zafarani. Wakati wa Noeli ni wakati wa vyakula vitamu vitamu, na mapishi haya ya pilau nimetengeneza kwa sababu hiyo tu. Ili pilau hii iwe inavyotakiwa, lazima utumie zafarani. Kama huna zafarani unaweza kutumia manjano.
Mlo huu ni wakuwatosha watu 6 au 8.

Viungo

  • kjm 2       Pilau masala
  • kkm 1       Mchele
  • mafuta ya kupikia mchele
  • kkm 1/2       vutunguu (viwe vimekatwa vidogo vidogo)
  • jm 1       vitunguu swahumu
  • kjm       tangawizi (iliyotwangwa)
  • kjm 2       pilau masala
  • kkm 1       korosho
  • kkm 1       zabibu kavu (raisins)
  • kjc 1/2       Zafarani (ama kjc 1/4 manjano)
  • kkm 2-3       knorr imechanganywa na maji
  • kkm 1/2       tui zito la nazi
  • kjc 1/2       chumvi ( onja kwanza maana knorr in chumvi)
  • kjm 1       Majani ya Mgiligilani (dhania)

Mapishi

  1. Bandika sufuria, tia mafuta kwenye moto wa kati. Ongeza mchele na vitunguu. Changanya mbaka mchele uwe mweupe na pia unachambuka chambuka.
  2. Ongeza kwenye sufuria vitunguu, tangawizi, na pilau masala. Endelea kuchanganya ili viungo visigande chini ya sufuria pia mbaka vitunguu swaumu viive. Ongeza zafarani.
  3. Kwenye chombo tofauti, changanya tui lamoto na mchuzi wa kuku wa moto
  4. Ongeza mchanganyiko huo wa nazi kwenye sufuria ya mchele ulio jikoni.
  5. Funika sufuria halafu punguza moto uwe kati ya moto wa katikati na wachini. Maji kama yakikauka ongeza korosho, changanya vizuri halafu ongeza nusu kikombe cha mchuzi wa kuku. Onja uone kama chumvi inatosha.
  6. Kama pilau ikikaribia kuiva, ongeza zabibu kavu, majani ya mgiligilani. Changanya vizuri, funika endelea kupika au weka kwenye oveni kama 300F mbaka ukauke vizuri.
  7. Weka mezani wakati bado pilau lina moto.
Chakula hiki ninaenda vizuri na: Kachumbari, na mchuzi wowote ule.

Tags: , , ,

34 Responses to Pilau La Noeli

  1. joan on January 27, 2012 at 2:03 am

    aina ya mapishi inatagemea na mtu mwenyewe.Pishi ni zuri na tamu. Jaribuni. tusikariri mapishi tubadilike wandugu

  2. Christmas Pilau (in video) | A Taste of Tanzania on December 23, 2011 at 8:56 am

    [...] did post this recipe for the first time in December 24 2009 in English and January 22 2010 in Swahili. A few people had hard time with it. I have decided to make a video so that those few people can [...]

  3. kemyta on July 7, 2011 at 11:02 am

    Habari mwalimu,
    I am sorry but when I follow your instructions to return to the rice option to find this recipe in english… i am only able to find it in swahili. please assist

  4. joyce on February 9, 2011 at 8:23 pm

    I love this recipe but am not very good in swahili,is it possible to have it in english.

    • Miriam Rose Kinunda on February 9, 2011 at 10:42 pm

      I do have this in English. At the top Menu Select Grain – -> then select Rice – -> then you will have different choices of rice recipes, choose Chrismas Menu. Download the pdf. One of the recipes in that pdf file is this pilau recipe in English

  5. [...] – Make a traditional Pilau with guidance from Miriam Rose Kinunda on A Taste of [...]

  6. [...] – Preparate un Pilau tradizionale [swa] sotto la guida di Miriam Rose Kinunda su A Taste of [...]

  7. Christmas Recipes in Global Food Blogs :: Elites TV on December 23, 2010 at 5:25 pm

    [...] – Make a traditional Pilau with guidance from Miriam Rose Kinunda on A Taste of [...]

  8. [...] – Make a traditional Pilau with guidance from Miriam Rose Kinunda on A Taste of [...]

  9. oleafrica on November 30, 2010 at 10:00 am

    Hiyo lazima niambie mke wangu ajaribu kuipika. Asante Bi Miriam.

    • NEEMA on January 6, 2011 at 6:01 am

      JAMANI HIYO PILAU NILILIPIKA XMAS ILIYOPITA,NI TAAMU SANA NA MUME WANGU KANISIFIA.ASANTE ENDELEZA MAFUNZO DADA.SIE WENGINE TWAPENDA MAPISHI

      • Miriam Rose Kinunda on January 10, 2011 at 6:27 pm

        Asante sana Neema, nashukuru mliipenda. Mimi najaribu kubadolisha mapishi yetu yawe rahisi kupika haraka. Watu wengi wanataka kila mtu apike kama babu zetu walivyokuwa wanapika zamani. Unless Mzungu aje aandike kifupi halafu tumsifu, tukifupisha sisi wenyewe tunajiona tunaaribu mapishi.

  10. zainab mrisho on November 30, 2010 at 8:13 am

    kila mtu na mawazo yake.kwa upande wangu mchele mmoja mapishi mbalimbali.mi naona pishi limetulia wadau.

  11. Sara on November 13, 2010 at 3:46 am

    mi naona chakula ni kizuri tu
    ahsante mpishi wetu

    wadau, vitunguu swaumu vimewekwa
    ukiangalia maelezo , amesema weka mchele na vitunguu hii ikimaanisha vitunguu maji na vitunguu saumu

    pia pinti ya kusema kwa nini aweke mchele na vitunguu sambamba..
    kwenye maandalizi amesema kata vitunguu vidogovidogo, hii ikiashiria yeye anapendezwa na hali kwamba vitunguu visiive sanaaa ndio raha ya pishi lake
    ni ubunifu tu wandugu
    na ndio raha ya jiko, kuwa mtundu

    ahsante, mi nimejipikia nikajionjea utamu.

  12. rubby on November 11, 2010 at 12:25 pm

    zafarani ni nini mamie????

  13. Tina on August 31, 2010 at 5:14 am

    Naungana na aliyesema mtiririko wa upishi si mzuri, pengine akiweka fresh mtiririko wake ni chakula kizuri pia

  14. Tina on August 31, 2010 at 5:12 am

    Wadau someni namba 2, mbona naona kama amesema vitunguu swaumu, pengine alichokosea ni kutaja wakati gani vinawekwa

  15. hidaya on August 11, 2010 at 11:45 am

    je pilau hiyo aiwekwi vituguu swaum

  16. Stella Mwakabuta on July 15, 2010 at 6:02 am

    Ni kweli pilau gani haihitaji kitunguu swaumu kweli hapo amechemsha kwa siye tunaojua mapishi tunaona hapo amechemsha

  17. layla on May 30, 2010 at 5:13 am

    ni kweli mtiririko wa mapishi si mzuri,uliona wapi kitunguu kinawekwa pamoja na mchelle??
    kwa siye tunaojua mapishi tunaona kabissa hapo ni utumbooooooo mtuuupu, SIJAPIKKA BADDOOOO!!!

    • Rose Kinunda on August 8, 2010 at 4:13 pm

      Layla,
      Mapishi yanatofautian kati ya watu na watu, ama nchi na nchi. Katika nchi zote nilizoishi, nimepata bahati ya kujifunza ingalau pishi moja la mchele ambalo pia lina vitunguu kama kiungo kimoja wapo. Sasa inategemea unaishi mji gani Tanzania, lakini najua kuwa mama aliyenifundisha kupika, anapenda sana vitunguu katika wali. Jaribu nahisi utapenda.

  18. Chiku on May 16, 2010 at 7:04 am

    Hii pilau ni nzuri..wadau mnajua mapishi hata kama ya kitanzania mara nyingi ni tofauti kidogo na hutegemea unatoka kona gani ya TZ. Maana pwani wanapika hivi na Arusha wanapika hivi..so cha msingi ni kupenda kujifunza mambo mapya..na kama kitu haupendi basi ignore it wengine watakipenda it is as easy as that..

  19. Chiku on May 16, 2010 at 7:03 am

    Hii pilau ni nzuri..wadau manajua mapishi hata kama ya kitanzania mara nyingi ni tofauti kidogo na hutegemea unatoka kona gani ya TZ. Maana pwani wanapika hivi na Arusha wanapika hivi..so cha msingi ni kupenda kujifunza mambo mapya..na kama kitu haupendi basi ignore it wengine watakipenda it is as easy as that..

  20. getrude deogratius on April 28, 2010 at 4:00 am

    mm nahitaji kujua mapishi ya aina mbalimbali

  21. Mimi on March 14, 2010 at 9:23 pm

    MImi ninafikiri Knorr ni Chicken Broth( Supu ya kuku inayotokana na kuchemshwa nyama ya kuku) halafu pia hii aina ya Pilau ni nzuri kwa kweli sielewi unasema mtiririko waupishi sio mzuri yaani una maana gani.

    • Rose Kinunda on August 8, 2010 at 4:16 pm

      WaTanzania wengine wanaita “Kidonge cha supu”. Asante Mimi

    • Rose Kinunda on August 8, 2010 at 4:17 pm

      WaTanzania wengine wanaita Kidonge cha supu. Asante Mimi

  22. mpishi 1 on February 8, 2010 at 1:17 pm

    Mpishi yoyote anayepika sana na anejua kupika, anajua knorr ni nini. zinapatikana madukani jijini Dar. Sijui huko nje, lakini mimi huwa nanunua mtaani kwetu.

  23. mpishi on February 4, 2010 at 7:28 pm

    Knor ndo nini kwa ufupi pilau ya ainahiyo si nzuri pili mtiririko waupishi si mzuri

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *


*




Archives

Facebook

RSS RSS

  • Is there any difference between mahamri and mandazi? May 10, 2013
    As I am reading my old notes here, I came across something that I wrote a few years ago but I forgot to post it here. Before I post this topic, I would like to hear what my readers have to say. When I used to live in Nairobi Kenya in my teenage years, I noticed that almost every Kenyan I knew did not know what mandazi were, but they did know mahamri. I used […]
    Miriam Kinunda