Pilau La Noeli

Friday, January 22, 2010
By Miriam Rose
 

 

 

 

 

 

  • kkm – Kikombe / vikombe
  • kjm – Kijiko cha meza / vijiko
  • kjc  – Kijiko cha chai / vijiko

Hili ni pilau tamu sana kwa sababu ya mchanganyiko wa korosho, zabibu kavu na zafarani. Wakati wa Noeli ni wakati wa vyakula vitamu vitamu, na mapishi haya ya pilau nimetengeneza kwa sababu hiyo tu. Ili pilau hii iwe inavyotakiwa, lazima utumie zafarani. Kama huna zafarani unaweza kutumia manjano.
Mlo huu ni wakuwatosha watu 6 au 8.

Viungo

  • kjm 2           Pilau masala
  • kkm 1          Mchele
  • mafuta ya kupikia mchele
  • kkm 1/2      vutunguu (viwe vimekatwa vidogo vidogo)
  • kjm 1          vitunguu swahumu
  • kjm              tangawizi (iliyotwangwa)
  • kjm 2           pilau masala
  • kkm 1          korosho
  • kkm 1          zabibu kavu (raisins)
  • kjc 1/2         Zafarani (ama kjc 1/4 manjano)
  • kkm 2-3      knorr imechanganywa na maji
  • kkm 1/2      tui zito la nazi
  • kjc 1/2        chumvi ( onja kwanza maana knorr in chumvi)
  • kjm 1          Majani ya Mgiligilani (dhania)

Mapishi

  1. Bandika sufuria, tia mafuta kwenye moto wa kati. Ongeza mchele na vitunguu. Changanya mbaka mchele uwe mweupe na pia unachambuka chambuka.
  2. Ongeza kwenye sufuria vitunguu, tangawizi, na pilau masala. Endelea kuchanganya ili viungo visigande chini ya sufuria pia mbaka vitunguu swaumu viive. Ongeza zafarani.
  3. Kwenye chombo tofauti, changanya tui lamoto na mchuzi wa kuku wa moto
  4. Ongeza mchanganyiko huo wa nazi kwenye sufuria ya mchele ulio jikoni.
  5. Funika sufuria halafu punguza moto uwe kati ya moto wa katikati na wachini. Maji kama yakikauka ongeza korosho, changanya vizuri halafu ongeza nusu kikombe cha mchuzi wa kuku. Onja uone kama chumvi inatosha.
  6. Kama pilau ikikaribia kuiva, ongeza zabibu kavu, majani ya mgiligilani. Changanya vizuri, funika endelea kupika au weka kwenye oveni kama 300F mbaka ukauke vizuri.
  7. Weka mezani wakati bado pilau lina moto.
Chakula hiki ninaenda vizuri na: Kachumbari, na mchuzi wowote ule.
 

 

 

 

 

 

 

Pilau la Noeli

Pilau la Noeli

Wakati wa Noeli umeisha, lakini kwa sababu wachache wamependelea nitafsiri mapishi yawe kwa Kiswahili. Nimeona ni vizuri nianze na pishi hili maan ni tamu sana. Na pia unaweza kuliandaa wakati wowote wa sherehe yoyote ile. Sasa, kurahisisha mambo, weka makini haya katika viungo
 

 

 

 

 

 

Tags: , ,

3 Responses to “Pilau La Noeli”

  1. mpishi

    Knor ndo nini kwa ufupi pilau ya ainahiyo si nzuri pili mtiririko waupishi si mzuri

    #255
  2. mpishi 1

    Mpishi yoyote anayepika sana na anejua kupika, anajua knorr ni nini. zinapatikana madukani jijini Dar. Sijui huko nje, lakini mimi huwa nanunua mtaani kwetu.

    #257
  3. Mimi

    MImi ninafikiri Knorr ni Chicken Broth( Supu ya kuku inayotokana na kuchemshwa nyama ya kuku) halafu pia hii aina ya Pilau ni nzuri kwa kweli sielewi unasema mtiririko waupishi sio mzuri yaani una maana gani.

    #281

Leave a Reply

Search Recipes

Subscribe

Archives

Categories